Thursday, July 3, 2008

WACHAPAKAZI WALIOSAHAULIKA

Naomba nianze mjadala huu kwa kuwapitisha kwenye mahojiano kati ya Bwana Macdonalds ambaye ni Mwekezaji toka Uingereza na Mzee Fungameza ambaye ni mlinzi katika kampuni ya Macdonalds. ENDELEA!!!
Macdonalds:Mkeo anafanya kazi gani bwn Fungameza?
Mzee Fungameza:Hafanyi kazi Boss!
Macdonalds:Akiamka asubuhi huwa anafanya nini?
Mzee Fungameza:Huwa anatandika kitanda,kufagia uwanja,kuwapikia watoto pamoja na mimi chai,kisha kuwasindikiza watoto shule na akirudi huenda kisimani kuchota maji.
Macdonalds:Mchana huwa anafanya nini?
Mzee Fungameza:Mchana huenda kuokota kuni za kupikia na kuhakikisha chakula kinakuwa tayari watoto wakirudi.
Macdonalds:Jioni huwa anafanya nini?
Mzee Fungameza:Jioni huwa anaenda kuchota maji ,anawaogesha watoto,ananichemshia maji ya kuoga na kupika chakula cha jioni
Macdonalds: Siku za weekend mkeo huwa anafanya nini?
Mzee Fungameza:huwa anapika kifungua kinywa,chakula cha mchana,chakula cha jioni,anafua nguo zangu,zake na za watoto,anaenda shamba na …
Macdonalds:Kwa hiyo mzee Fungameza mkeo anafanya kazi gain?
Mzee Fungameza:HAFANYI KAZI BOSS NADHANI NIMESHAKUAMBIA MAPEMA
Macdonalds: MY GOD!!!

Naam, hakuna ubishi kwamba kuna watu wengi ,wanaume kwa wanawake wenye mawazo kama ya Mzee Fungameza ambao kwao kazi ni ile shughuli inayompatia mtu malipo/vijisenti ya moja kwa moja. Kwa hiyo kwao kazi isiyoambatana na malipo ya moja kwa moja sio KAZI,ila kwa kazi zenye malipo ya moja kwa moja kama kazi aifanyayo Mzee Fungameza ndio kazi bila kujali ni kiasi gani analeta nyumbani kwisho wa mwezi.Ni kwa bahati mbaya sana kwamba jamii imezipachika jina kazi zisizokuwa na malipo ya moja kwa moja kuwa ni za WANAWAKE.kwa hiyo kazi zifanyikazo majumbani kwetu kama kufua,kufagia,kudeki,kuosha vyombo,kuogesha watoto,kutafuta kuni,kuchota maji,kupika nk huonekana kuwa ni za kike.Watoto wanazaliwa katika jamii hizi na kujikuta wakiendeleza dhana hii ambayo mi naiona potofu.Ah,mama mi nikadeki kwani mimi ni mwanamke?atasikika mototo wa kiume akisema hivyo.Haishangazi kuwa wanaume walioa wakikutwa wanafanya kazi hizo huonekana WAMEKAMATWA,WAMELISHWA LIMBWATA,WAMEKALIWA nk.Inashangaza kuwa wanawake ndio huwa wa kwanza kuwashutumu wanaume (kaka zao/wadogo zao) wanapowaona wanafanya kazi hizo ‘za kike’ badala ya kuwaunga mkono na kuwapa moyo kwa ushirikiano mzuri katika ndoa zao.Lakini cha kushangaza ni pale kazi hizi hizi ‘za kike’ zinapohusisha malipo ya moja kwa moja/vijisenti, wanaume huzikimbilia,huzipora na kuzimiliki.WHY??/KWANINI???inawezekana labda sieleweki! Nina maanisha UDOBI (iwe dobi wa mtaani au dry cleaner-huku ni kufua nguo),UPISHI MAHOTELINI-kupika ni kupika tu,UUZAJI MAJI MITAANI-huku ni kuchota maji,UUZAJI KUNI NA MKAA-huku ni kutafuta kuni,UFAGIZI MASOKONI/BARABARANI/MAOFISINI-huku nikufagia N.K.Tuko pamoja?kwa hiyo hapa swala la kazi za ‘kike” wala kazi za ‘kiume’ halipo.kilicho dhahiri ni kwamba jamii haiheshimu kazi kubwa wazifanyazo dada/mama(hasa wa vijijini) zetu kutwa nzima bila kupumzika.Ukitaka kujua kuwa wanawake huchangia kiasi kikubwa sana cha pesa katika maendeleo ya familia zetu basi ajili watu/mtu wa kufanya kazi zote anazofanya mwanamke kwa siku nyumbani halafu uone utachajiwa kiasi gani.Hapo utaona ni kiasi gani cha pesa huyu kiumbe jasiri amekiokoa.Karibuni wadau,mjadala uko wazi,mawazo yenu ni muhimu katika katika kuondoa fikra potofu iliyojikita katika jamii yetu ya kutoheshimu mchango wa wanawake(hasa mwanamke wa kiafrika) katika maisha yetu ya kile siku…welcome

No comments: